
Waasi wa M23 wamesalimu amri baada ya kupata kipigo kikali
Waasi wa M23 katika Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wametangaza kumaliza uasi wao ndani ya nchi hiyo muda mfupi baada ya kupigwa katika ngome yao ya mwisho na majeshi ya serikali ya Congo yakishirikiana na kikosi maalum cha Umoja wa Mataifa kilichopewa uwezo wa kupigana na waasi hao.